Latest

MASOMO YA MISA, OKTOBA 1, 2017 DOMINIKA YA 26 YA MWAKA A MWANZO: Dan. 3:31, 29, 30, 43, 42 Ee Bwana, yote uliyotutendea, umeyatenda kwa haki, kwa kuwa sisi tumetenda dhambi, wala hatukuzitii amri zako. Ulitukuze jina lako na kututendea sawasawa na wingi wa huruma zako. SOMO 1 Eze. 18:25-28 Bwana ameniambia hivi: Ninyi mwasema, Njia ya Bwana si sawa. Sikiliza sasa, Enyi nyumba ya Israeli; Je! Njia yangu siyo iliyo sawa? Njia zenu sizo zisizo sawa? Mwenye haki atakapoghairi, na kuiacha haki yake, na kutenda uovu, atakufa katika uovu huo; katika uovu wake alioutenda atakufa. Tena, mtu mwovu atakapoghairi, na kuuacha uovu wake alioutenda, na kutenda yaliyo halali na haki, ataponya roho yake, nayo itakuwa hai. Kwa sababu atafakati, na kughairi, na kuyaacha makosa yake yote aliyoyatenda, hakika, ataishi, hatakufa. Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu. WIMBO WA KATIKATI Zab. 25:4-9, (K) 6 (K) Kumbuka rehema zako, Ee Bwana. Ee Bwana, unijulishe njia zako, Unifundishe mapito yako; Uniongoze katika kweli yako, Na kunifundisha: Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu. (K) Ee Bwana, kumbuka rehema zako na fadhili zako. Maana zimekuwako tokea zamani. Usiyakumbuke makosa ya ujana wangu, Wala mausi yangu, Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili zako, Ee Bwana, kwa ajili ya wema wako. (K) Bwana yu mwema, mwenye adili, Kwa hiyo atawafundisha njia wenye dhambi. Wenye upole atawaongoza katika hukumu. Wenye upole atawafundisha njia yake. (K) SOMO 2 Flp. 2:1-11 Ikiwako faraja yoyote katika Kristo, yakiwako matulizo yoyote ya mapenzi, ukiwako ushirika wowote wa Roho, ikiwako huruma yoyote na rehema, ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja. Msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo yaw engine. Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba. Neno la Bwana…Tumshukuru Mungu. SHANGILIO Yn. 15:15 Aleluya, aleluya Ninyi nimewaita rafiki, kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu. Aleluya. INJILI Mt. 21:28-32 Yesu aliwaambia wakuu wa makuhani na wazee, Mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu. Akajibu akasema, naenda, Bwana; asiende. Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda. Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili. Bwana Yesu akawaambia, Amin, nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu. Kwa sababu Yohana alikuja kwenu kwa njia ya haki, ninyi msimwamini; lakini watoza ushuru na makahaba walimwamini; nanyi hata mlipoona, hamkutubu baadaye, ili kumwamini. Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

MASOMO YA MISA, OKTOBA 1, 2017
DOMINIKA YA 26 YA MWAKA A

MWANZO:
Dan. 3:31, 29, 30, 43, 42
Ee Bwana, yote uliyotutendea, umeyatenda kwa haki, kwa kuwa sisi tumetenda dhambi, wala hatukuzitii amri zako. Ulitukuze jina lako na kututendea sawasawa na wingi wa huruma zako.

SOMO 1
Eze. 18:25-28

Bwana ameniambia hivi: Ninyi mwasema, Njia ya Bwana si sawa. Sikiliza sasa, Enyi nyumba ya Israeli; Je! Njia yangu siyo iliyo sawa? Njia zenu sizo zisizo sawa? Mwenye haki atakapoghairi, na kuiacha haki yake, na kutenda uovu, atakufa katika uovu huo; katika uovu wake alioutenda atakufa. Tena, mtu mwovu atakapoghairi, na kuuacha uovu wake alioutenda, na kutenda yaliyo halali na haki, ataponya roho yake, nayo itakuwa hai. Kwa sababu atafakati, na kughairi, na kuyaacha makosa yake yote aliyoyatenda, hakika, ataishi, hatakufa.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 25:4-9, (K) 6

(K) Kumbuka rehema zako, Ee Bwana.

Ee Bwana, unijulishe njia zako,
Unifundishe mapito yako;
Uniongoze katika kweli yako,
Na kunifundisha:
Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu. (K)

Ee Bwana, kumbuka rehema zako na fadhili zako.
Maana zimekuwako tokea zamani.
Usiyakumbuke makosa ya ujana wangu,
Wala mausi yangu,
Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili zako,
Ee Bwana, kwa ajili ya wema wako. (K)

Bwana yu mwema, mwenye adili,
Kwa hiyo atawafundisha njia wenye dhambi.
Wenye upole atawaongoza katika hukumu.
Wenye upole atawafundisha njia yake. (K)

SOMO 2
Flp. 2:1-11

Ikiwako faraja yoyote katika Kristo, yakiwako matulizo yoyote ya mapenzi, ukiwako ushirika wowote wa Roho, ikiwako huruma yoyote na rehema, ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja. Msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo yaw engine. Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.

Neno la Bwana…Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO
Yn. 15:15

Aleluya, aleluya
Ninyi nimewaita rafiki, kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.
Aleluya.

INJILI
Mt. 21:28-32

Yesu aliwaambia wakuu wa makuhani na wazee, Mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu. Akajibu akasema, naenda, Bwana; asiende. Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda. Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili. Bwana Yesu akawaambia, Amin, nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu. Kwa sababu Yohana alikuja kwenu kwa njia ya haki, ninyi msimwamini; lakini watoza ushuru na makahaba walimwamini; nanyi hata mlipoona, hamkutubu baadaye, ili kumwamini.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

MASOMO YA JUMAPILI OCTOBER 1

MASOMO YA MISA, OKTOBA 1, 2017
DOMINIKA YA 26 YA MWAKA A

MWANZO:
Dan. 3:31, 29, 30, 43, 42
Ee Bwana, yote uliyotutendea, umeyatenda kwa haki, kwa kuwa sisi tumetenda dhambi, wala hatukuzitii amri zako. Ulitukuze jina lako na kututendea sawasawa na wingi wa huruma zako.

SOMO 1
Eze. 18:25-28

Bwana ameniambia hivi: Ninyi mwasema, Njia ya Bwana si sawa. Sikiliza sasa, Enyi nyumba ya Israeli; Je! Njia yangu siyo iliyo sawa? Njia zenu sizo zisizo sawa? Mwenye haki atakapoghairi, na kuiacha haki yake, na kutenda uovu, atakufa katika uovu huo; katika uovu wake alioutenda atakufa. Tena, mtu mwovu atakapoghairi, na kuuacha uovu wake alioutenda, na kutenda yaliyo halali na haki, ataponya roho yake, nayo itakuwa hai. Kwa sababu atafakati, na kughairi, na kuyaacha makosa yake yote aliyoyatenda, hakika, ataishi, hatakufa.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 25:4-9, (K) 6

(K) Kumbuka rehema zako, Ee Bwana.

Ee Bwana, unijulishe njia zako,
Unifundishe mapito yako;
Uniongoze katika kweli yako,
Na kunifundisha:
Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu. (K)

Ee Bwana, kumbuka rehema zako na fadhili zako.
Maana zimekuwako tokea zamani.
Usiyakumbuke makosa ya ujana wangu,
Wala mausi yangu,
Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili zako,
Ee Bwana, kwa ajili ya wema wako. (K)

Bwana yu mwema, mwenye adili,
Kwa hiyo atawafundisha njia wenye dhambi.
Wenye upole atawaongoza katika hukumu.
Wenye upole atawafundisha njia yake. (K)

SOMO 2
Flp. 2:1-11

Ikiwako faraja yoyote katika Kristo, yakiwako matulizo yoyote ya mapenzi, ukiwako ushirika wowote wa Roho, ikiwako huruma yoyote na rehema, ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja. Msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo yaw engine. Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.

Neno la Bwana…Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO
Yn. 15:15

Aleluya, aleluya
Ninyi nimewaita rafiki, kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.
Aleluya.

INJILI
Mt. 21:28-32

Yesu aliwaambia wakuu wa makuhani na wazee, Mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu. Akajibu akasema, naenda, Bwana; asiende. Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda. Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili. Bwana Yesu akawaambia, Amin, nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu. Kwa sababu Yohana alikuja kwenu kwa njia ya haki, ninyi msimwamini; lakini watoza ushuru na makahaba walimwamini; nanyi hata mlipoona, hamkutubu baadaye, ili kumwamini.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

MASOMO YA MISA JUMANNE.

MASOMO YA MISA, SEPTEMBA 26, 2017
JUMANNE, JUMA LA 25 LA MWAKA

SOMO 1
Ezr. 6:7-8, 12, 14-20

Mfalme Dario alimwandikia liwali wa ng’ambo wa mto, na wenzake; Waacheni liwali wa Wayahudi na wazee wa Wayahudi, waijenge nyumba hii ya Mungu mahali pake. Tena, natoa amri kuwaagiza ninyi mtakayowatendea wazee hao wa Wayahudi kwa kazi hii ya kuijenga nyumba ya Mungu; katika mali ya mfalme, yaani, katika kodi za nchi iliyo ng’ambo ya Mto, watu hao wapewe gharama zote kwa bidii, ili wasizuiliwe. Na Mungu huyu, aliyelifanya jina lake likae pale, na aangamize wafalme wote, na watu wote, watakonyosha mikono yao kulibadili neno hili, na kuiharibu nyumba hii ya Mungu, iliyoko Yerusalemu. Mimi, Dario, nimetoa amri; na ifanyike kwa bidii nyingi. Nao wazee wa Wayahudi wakajenga, wakafanikiwa, kwa masaada wa kuhubiri kwao Hagai nabii, na Zekaria mwana wa Ido.
Wakajenga, wakaimaliza kazi yao, kwa maagizo ya Mungu wa Israeli, na kwa amri ya Koreshi, na Dario, na Artashasta mfalme wa Uajemi. Nyumba hiyo ikamalizika siku ya tatu ya mwezi Adari, katika mwaka wa sita wa kutawala kwake mfalme Dario. Na wana wa Israeli, na makuhani, na walawi na watu wengine katika hao waliohamishwa, wakaiweka wakfru nyumba ya Mungu kwa furaha. Na katika kuiweka wakfu nyumba ya Mungu, wakatoa sadaka, ng’ombe mia, na kondoo waume mia mbili, na wanakondoo mia nne; tena wakatoa mbuzi waume kumi na wawili, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli wote, kwa hesabu ya kabila za Israeli. Wakawaweka makuhani katika kura zao, wakawaweka na Walawi vilivyoandikwa katika chuo cha Musa. Kisha, wana wa uhamisho wakaifanya Pasaka, mwezi wa kwanza, siku ya kumi nan ne ya mwezi. Kwa maana makuhani na Walawi walikuwa wamejitakasa wote pamoja; wote walikuwa hali ya tohara; wakachinja pasaka kwa ajili ya wana wote wa uhamisho, na kwa ajili ya ndugu zao makuhani, na kwa ajili ya nafsi zao.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 122:1-5 (K) 1

(K) Nalifurahi waliponiambia, na twende nyumbani kwa Bwana.

Nalifurahi waliponiambia,
Na twende nyumbani kwa Bwana. (K)

Miguu yetu imesimama
Ndani ya malango yako, ee Yerusalemu!
Ee Yerusalemu uliyejengwa
Kama mji ulioshikamana. (K)

Huko ndiko walikopanda kabila,
Kabila za Bwana;
Ushuhuda wa Israeli,
Walishukuru jina la Bwana.
Maana huko viliwekwa viti vya hukumu,
Viti vya enzi vya mbari ya Daudi. (K)

SHANGILIO
1Pet. 1:25

Aleluya, aleluya,
Neno la Bwana hudumu hata milele, na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa kwenu.
Aleluya.

INJILI
Lk. 8:19 – 21

Walimwendea Yesu mama yake na ndugu zake, wasiweze kumkaribia kwa sababu ya mkutano. Akaletewa habari akiambiwa, Mama yako na ndugu zako wamesimama nje wakitaka kuonana nawe. Akawajibu akasema, Mama yangu na ndugu zangu ndio hao walisikiao neno la Mungu na kulifanya.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

TAFAKARI YA LEO JUMATATU

“ASLI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumatatu, Septemba 25, 2017.
Juma la 25 la mwaka

Ezra 1: 1-6;
Zab 126;
Lk 8:16-18

WEWE NI NURU: ANGAZA

Wakati jua linapo zama na giza kuingia, mwanga unaleta tena maisha, na kunakuwa na mizunguko mingine na kazi huendelea. Yesu leo analiweka wazi, kumwamini yeye na kumfuata haipaswi kuwa na moyo nusu nusu na haipaswi kuwa kitu cha “siri” kwamba unakuwa unaona aibu kwasababu ya wengine. Kama wanafunzi wa Yesu hatupaswi kuwa na wasi wasi wowote au kuogopa wengine wanasema nini juu yetu. Hata hivyo, tunatafuta Amani, upendo, msamaha, haki na thamani ya Injili; tunapaswa kutembea tukiwa na ujasiri wote. Tujiringie kuwa wabebaji wa mwanga mkuu-YESU. Haijalishi tutapita katika giza lipi, ulimwengu wenye mashaka, sisi tunao mwanga wenye kuangaza njia zetu mpaka mwisho. Inaweza kuwa ngumu lakini tunapaswa kutembea katika mwanga huu tukifanya kazi na kusonga mbele. Mpaka pale tutakapo kuwa na mwanga huu milele, tusiogope na wala tusipoteze tumaini la mema tutakayo pata kwa hili.

Ukweli huu halisi ni chanzo cha mangamuzi yetu kuhusu uhusiano wetu na Kristo. Katika kweli kama Yesu yupo kweli katika maisha yetu, kama tunaishi maisha ya upendo wa kweli naye, tutaweza kuona matokeo kwa wale tunao ishi nao karibu yetu. Tutaweza kuona mwanga ukiwaangazia wengine. Matokeo ya Yesu kuangaza kupitia sisi itakuwa kama kioo kwa mioyo yetu.

Angalia. Kama watu wanavutwa na upendo wa Kristo kupitia wewe. Kama sio, angalia ndani ya moyo wako na washa tena moto wa upendo wa Mungu . Tufurahi kwamba sisi tunabeba mwanga mkubwa-Yesu. Ulimwengu wenye giza unahitaji mwanga wa Kristo.

Sala: Bwana, njoo washa ndani mwangu, uweke moyo wangu kwenye mapendo kwa upendo wako. Ninatamani moyo wangu uwe chemchemi ya kuwavuta watu kwako. Bwana nitumie mimi kama upendavyo. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

MASOMO YA JUMATATU.

MASOMO YA MISA, SEPTEMBA 25, 2017
JUMATATU, JUMA LA 25 LA MWAKA

SOMO 1
Ezr. 1:1-6

Ilikuwa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalame wa Uajemi, ili kwamba neno la Bwana alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, Bwana akamwambia roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia akisema,
Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi: Bwana Mungu wa mbinguni amenipa falme zote za dunia; naye ameniagiza nimjengee nyumba katika Yerusalemu, ulioko Yuda. Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, Mungu wake na awe pamoja naye, na akwee mpaka Yerusalemu, ulioko Yuda, akaijenge nyumba ya Bwana, Mungu wa Israeli, (yeye ndiye Mungu), iliyoko Yerusalemu. Na mtu awaye yote aliyesalia mahali popote akaapo hali ya ugeni, na asaidiwe na watu wa mahali pake, kwa fedha, na dhahabu, na mali, na wanyama, zaidi ya vitu vitolewavyo kwa hiari ya mtu, kwa ajili ya nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu.
Ndipo wakaondoka wakuu wa mbari za mababa, wa Yuda na Benyamini, na makuhani, na Walawi, naam, watu wote ambao Mungu amewaamsha roho zao kukwea, ili kuijenga nyumba ya Bwana, iliyoko Yerusalemu. Na watu wote, waliokaa karibu nao pande zote wakawatia nguvu mikono yao, kwa vyombo vya fedha, kwa dhahabu, kwa mali, na kwa wanyama, na vitu vya thamani, zaidi ya vile vilivyotolewa kwa hiari ya mtu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 126 (K) 3

(K) Bwana alitutendea mambo makuu.

Bwana alipowarejeza mateka wa Sayuni,
Tulikuwa kama waotao ndoto.
Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko,
Na ulimi wetu kelele za furaha.
Ndipo waliposema katika mataifa,
“Bwana amewatendea mambo makuu”. (K)

Bwana alitutendea mambo makuu,
Tulikuwa tukifurahi.
Ee Bwana, uwarejeze watu wetu waliofungwa,
Kama vijito vya Kusini. (K)

Wapandao kwa machozi
Watavuna kwa kelele za furaha.
Ingawa mtu anakwenda zake akilia,
Azichukuapo mbegu za kupanda,
Hakika atarudi kwa kelele za furaha,
Aichukuapo miganda yake. (K)

SHANGILIO
Yak. 1:18

Aleluya, aleluya,
Kwa kupenda kwake mwenyewe, Baba alituzaa sisi kwa neno la kweli, tuwe kama limbuko la viumbe vyake.
Aleluya.

INJILI
Lk. 8:16 – 18

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Hakuna mtu ambaye akiisha washa taa huifunika kwa chombo, au kuiweka uvunguni, bali huiweka juu ya kiango, ili waingiao wapate kuona nuru yake. Kwa maana hakuna neno lililositirika ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa ambalo halitajulikana na kutokea wazi. Jiangalieni basi jinsi msikiavyo; kwa kuwa mwenye kitu atapewa, na yule asiye na kitu atanyang’anywa hata kile ambacho anadhaniwa kuwa nacho.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo

MASOMO YA MISA, SEPTEMBA 24, 2017
DOMINIKA YA 25 YA MWAKA A

MWANZO:
Bwana asema: Mimi ni wokovu wa watu. Wakinililia katika taabu yoyote nitawasikiliza, nami nitakuwa Bwana wao milele.

SOMO 1
Isa. 55:6 – 9

Mtafuteni Bwana, maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yu karibu;
Mtu mbaya na aache njia yake, Na mtu asiye haki aache njia yake, Na mtu asiye haki aache mawazo yake; na amrudie Bwana. Naye atamrehemu; Na arejee kwa Mungu wetu, Naye atamsamehe kabisa.
Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema Bwana. Kwa maana kwa vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 145:2-3, 8-9, 17-18 (K) 18

(K) Bwana yu karibu na wote wamwitao.

Kila siku nitakuhimidi,
Nitalisifu jina lako milele na milele.
Bwana ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana,
Wala ukuu wake hautambulikani. (K)

Bwana ana fadhili ni mwingi wa huruma,
Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema.
Bwana ni mwema kwa watu wote;
Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote. (K)

Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote,
Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote.
Bwana yu karibu na wote wamwitao,
Wote wamwitao kwa uaminifu. (K)

SOMO 2
Flp. 1:20-24, 27

Kristu ataadhimishwa katika mwili wangu; ikiwa kwa maisha yangu, au ikiwa kwa mauti yangu. Kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida. Ila ikiwa kuishi katika mwili, kwangu mimi ni matunda ya kazi; basi nitakalolichagua silitambui.
Ninasongwa katikati ya mambo mawili; ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo; maana ni vizuri Zaidi sana; bali kudumu katika mwili kwahitajiwa Zaidi kwa ajili yenu. Lakini mwenendo wenu na uwe kama inavyoipasa Injili ya Kristo.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO
Yn. 1:12, 14

Aleluya, aleluya,
Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; Wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu.
Aleluya.

INJILI
Mt. 20:1-16

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba, aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu. Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu. Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi; na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda. Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile. Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi? Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu. Kulipokuchwa, yule bwana wa shamba akamwambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu. Kulipokuchwa, yule bwana wa shamba akamwambia msimamizi wake, Waite wakulima, uwalipe ujira wao, ukianzia wa mwisho hata wa kwanza. Na walipokuja wale wa saa kumi na moja, walipokea kila mtu dinari. Na wale wa kwanza walipokuja, walidhani kwamba watapokea Zaidi; na hao pia wakapokea kila mtu dinari. Basi wakiisha kuipokea, wakamnung’unikia mwenye nyumba, wakisema, Hao wa mwisho wametenda kazi saa moja tu, nawe umewasawazisha na sisi tuliostahimili taabu na hari za mchana kutwa. Naye akamjibu mmoja wao, akamwambia, Rafiki, sikudhulumu; hukupatana nami kwa dinari? Chukua iliyo yako, uende zako; napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe. Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema? Vivyo hivyo wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

MASOMO YA DOMINIKA YA LEO.

MASOMO YA MISA,*
JUMAPILI, SEPTEMBA 17, 2017
JUMA LA 24 LA MWAKA
________

MWANZO
YbS 36:15.16

Ee Bwana, uwape amani wakungojao, ili watu wawasadiki manabii wako; usikilize sala ya mtumwa wako, na ya taifa lako Israeli.
________

SOMO I
YbS 27:30-28:1-7

Hasira na ghadhabu, haya pia ni machukuzo na aliye mwenye dhambi yatampata. Mwenye kujilipiza kisasi ataona kisasi kutoka kwa Bwana; hakika Yeye atamfungia dhambi zake. Umsamehe jirani yako dhara alilokufanyia, hivyo nawe utasamehewa dhambi zako wakati utakaposali. Mwanadamu humkasirikia mwanadamu, je! atatafuta kuponywa na Bwana? Hamrehemu mwanadamu aliye mwenzake, je! atalalamika kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe? Aliye mwili na damu tu huilisha hasira yake, je! ni nani atakayempatanisha yeye kwa makosa yake? Basi kumbuka mwisho wako, uuache uadui; kumbuka uozi na mauti , ujiepushe na kutenda dhambi. Kumbuka zile amri, usikasirike na jirani yako; nawe ulikumbuke agano lake Aliye juu, umwachilie ujinga wake.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 103:1-4, 9-12

(K) Bwana amejaa huruma na neema,
si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa fadhili.

Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,
Naam, vyote vilivyo ndani yangu
Vilihimidi jina lake takatifu.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,
Wala usizisahau fadhili zake zote. (K)

Ndiye anayekusamehe maovu yako yote,
Akuponya magonjwa yako yote.
Akomboa uhai wako na kaburi,
Akutia taji ya fadhili na rehema. (K)

Yeye hatateta siku zote,
Wala hatashika hasira yake milele.
Hatutendei kadiri ya hatia zetu,
Wala halipi kwa kadiri ya maovu yetu. (K)

Maana vile mbingu zilivyoinuka juu ya nchi,
Kadiri ile ile rehema zake ni kuu kwa wamchao.
Kama mashariki ilivyo mbali ma magharibi,
Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi. (K)
________

SOMO 2
Rum. 14:7-9

Hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa nafsi yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake. Kwa maana kama tukiishi, twaishi kwa Bwana, au kama tukifa, twafa kwa Bwana. Basi kama tukiishi au kama tukifa, tu mali ya Bwana. Maana Kristo alikufa akawa hai tena kwa sababu hii, awamiliki waliokufa na walio hai pia.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________

SHANGILIO
Yn. 13:34

Aleluya, aleluya,
Amri mpya nawapa, asema Bwana,
mpendane, kama vile nilivyowapenda ninyi.*_
Aleluya.

________

INJILI
Mt. 18:21-35

Petro alimwendea Yesu akamwambia, Bwana ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? hata mara saba? Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.
Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake. Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi. Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, akalipwe ile deni. Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia. Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni. Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia; akamkamata, akamshika koo, akisema, Nilipe uwiwacho. Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia. Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa deni. Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka. Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi; nawe, je! haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe? Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote. Ndiyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
 
Copyright ©2017 CATHOLIC FAITH GROUP • All Rights Reserved.
Design by innocent